
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika ziara ya kutembelea Kijiji
cha Nyamanzi na Dimani Sheha wa Shehia ya Nyamanzi Seif Muhammed Hassan
amesema mbali na uwepo wa ulinzi shirikishi katika maeneo yao lakini
wanashindwa kukabiliana na hali hiyo kutokana na kukosa vifaa vya
kitaalamu vya kulindia maeneo hayo.
Hata hivyo amesema mara kwa mara wamekuwa wakishuhudia Bidhaa mbali
mbali za magendo zinaletwa ikiwemo Mbao za kujengea pamoja na Madawa ya
kulevya ambayo ni hatari kwa vijana wao.
Aidha amesema pindipo Serikali itaimarisha ulinzi katika maeneo ya
ukanda wa bahari itasaidia kuwakamata kirahisi watu wanaoingizwa bidhaa
kinyume na sheria zilizowekwa.
Ziara hiyo ya siku moja iliandaliwa na Clab ya Waandishi wa Habari
Zanzibar ZPC kwa wandishi wa habari kutembelea Shehia za Dimani na
Nyamanzi kwa lengo la kujua umuhimu wa kuandika habari za Vijiji ikiwa
ni sehemu ya Shamrashamra ya kuadhimisha Siku ya uhuru wa Vyombo vya
habari nchini.
Nchanzo: Zanzibar24.
Comments