Wanajeshi 9 wa Chad wauawa katika shambulio la Boko Haram.

Kundi la Boko Haram limefanya shambulio dhidi ya kambi moja ya jeshi nchini Chad na kuua wanajeshi 9 wa nchi hiyo.

Hayo yameelezwa na msemaji wa jeshi la Chad ambaye amebainisha kwamba, kambi ya jeshi iliyoshambuliwa na wanamgambo wa Boko Haram ipo katika eneo linalopakana na Nigeria.

Kanali Azem Bermandoua ameeleza kuwa, mbali na wanajeshi wao wanane kuuawa katika shambulio hilo, kuna wengine 28 waliojeruhiwa pia katika hujuma hiyo ya kijeshi ya Boko Haram.

Jeshi la Chad limeeleza kuwa, limeimarisha usalama katika maeneo hayo baada ya shambulio hilo la wanamgambo wa Boko Haram wenye makao yao nchini Nigeria.
 
Shambulio hilo la Boko Haram linafanyika masaa kadhaa tu baada ya António Guterres Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kulitaka kundi la kigaidi la Boko Haram la nchini Nigeria kuhitimisha ukiukaji wake wa haki za watoto.

Kundi la Boko Haram lilianzisha mashambulizi dhidi ya maeneo ya umma na taasisi za serikali huko kaskazkini mwa Nigeria mwaka 2009 na baadaye mwaka 2015 likapanua mashambulizi hayo hadi katika nchi za Chad, Cameroon na Niger.

Zaidi ya watu elfu 20 wameuwa hadi sasa katika mashambulizi hayo na mamilioni ya wengine wamelazimika kuwa wakimbizi.
 chanzo:parstoday.

Comments