Wakulima wa
mwani mkoa wa kaskazini pemba wamekabidhiwa boti kumi[10] ambazo zitasaidakuendeleza
shughuli zao za kilimo chao.
Akikabidhi boti hizo Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba OMAR KHAMIS OTHMAN amesema
lengo la kukabidhi boti hizo ni kuendeleza Kilimo cha Mwani na kujiongezea
kipato katika familia zao.
Aidha amewataka wakulima hao kujipanga na kuhakikisha Boti hizo wanazifanyia
ukarabati kwa kutumia nguvu zao ili ziweze kudumu na kutumika kwa muda
mrefu huku akiwasisitiza kutoziuza.
Wakizungumza na mara baada ya kukabidhiwa boti hizo
kwa Niaba ya wakulima wenzao SHAIBU KASSIM HAMAD na KHADIJA WILSON
MAIGE wamesema Boti hizo zitawawezesha kuongeza uzalishaji wa zao la mwani.
Sambamba na hayo,wakulima hao wamesema kwamba zao la Mwani limewatia hasara
kubwa kutokana na msimu huu wa mvua kwani baada ya kuuwanika huchelewa kukauka
na hatimae huoza majumbani mwao kutokana na kukosa jua la kutosha.
Mara kwa Mara wakulima wa mwani Kisiwani Pemba hukabidhiwa vifaa mbali mbali
kwa ajili ya kupambana na Kilimo hicho ili kuweza kupata mavuno bora kwa ajili
ya kujikimu kimaisha.
Comments