Wajasiriamali na wafanyabiashara Kisiwani Pemba wafundwa.

Waziri wa Mambo yanje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Augustine Mahiga amewataka wajasirimali Kisiwani Pemba kuzutumia vyema fursa zilizopo ili kuweza kumudu ushindani katika soko la Afrika Mashari.




Waziri Mahiga ameyasema hayo wakati akifungua semina ya siku nne  kuhusu utoaji wa elimu kwa wajasiriamali na wafanya biashar  juu ya mtangamano wa Jumuiya Afrika Mashariki ambayo imefanyika katika ukumbi wa kiwanja cha Gombani Kisiwani Pemba.



Amesema kuwa wajasirimali na wafanyabiashara wanafursa kubwa zitakazo wasaidia kuingia katika soko la pamoja kutokana na kuwa nchi ya Tanzania ndio inayo ongoza kwa utoaji wa bidhaa bora zenyekuzingatia vigezo vinavyo hitajika.



Amefahamisha kuwa kuundwa kwa Soko  la Jumuiya ya Afrika Mashariki nikuwawezesha wajasiriamali na wafanya bishara hao kuweza kuongeza ushindani kwa nchi zinazo unda shirkisho hilo.

Nae naibu Warizi wa Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Zanzibar Mh Khamis Juma Maalim amesema kuwa Zanzibar imepiga hatua kubwa tangu kuanzishwa kwa soko la pamoja kwani limeweza kuwasaidia wajasiriamali kuweza kushiriki katika maonyesho mbali mbali hususan yale yanayo wahusu wajasiriamali.



Aidha ameeleza kuwa nimuda muwafaka kwa wajasirimali na wafanya biashara Kisiwani Pemba kuyatumia vyema mafunzo yao ili yaweze kuwaletea mabadiliko katika shughuli zao.



Kwaupande wake Mwenyekiti wa Soko la Jumapili Chake Chake Pemba Khamis Suleiman  Masoud kwaniaba ya wafanya biashara na wajasiriamali wenzake wameishukuru Serekali ya Mapinduzi Zanzibar na ile ya Muungano kwa kuwapatia mafunzo yatakayo wawezesha kubuni miradi itakayo wasaidia kuitangaza vyema tanzania na kuahidi kuyatumia ipasavyo mafunzo hayo.



Comments