Wahajiri 34, aghlabu yao watoto, wazama baharini Libya-ASU.

Wahajiri wasiopungua 34, wengi wao wakiwa ni watoto, walizama jana Jumatano katika Bahari ya Mediterranean karibu na pwani a Libya.

Waokoaji wanasema boti kadhaa zilikumbwa na dhoruba na kuzama ghafla zikiwa na abiria karibu 200. 

Kamanda wa Gadi ya Pwani ya Italia, Cosima Nicastro amesema, wameopoa miili 20 majini huku kundi la uokoaji la MOAS likisema limepata miili 34 aghlabu yao wakiwa ni watoto wadogo. 


Waokoaji wanasema, karibu boti 15 zilizokumbwa na dhoruba zilikuwa na abiria karibu 1,700.

Mwaka huu karibu watu 1,300 wamepoteza maisha mwaka huu wakivuka moja ya maeneo hatari zaidi baharini kwa lengo la kukimbia umasikini na vita barani Afrika na Mashariki ya Kati.

 Habari zinasema kuwa, mwaka jana zaidi ya wahajiri 5,000 hususan wa Kiafrika walipoteza maisha kwa kuzama baharini katika bahari ya Mediterania wakiwa katika safari hizo hatari za kuelekea Ulaya wanakodhani kwamba watapata maisha mazuri na ajira.
chanzo:parstoday.

Comments