Vitabu vya kiada vilivyobainika kuwa na makosa mengi ya usanifu,
picha za vitabu kucheza na makosa ya lugha, ni vya darasa la kwanza hadi
la tatu, lakini pia vimo vya sekondari. Alitoa msimamo huo wa Serikali
jana wakati akiwasilisha bajeti ya wizara yake mjini hapa.
Alisema, pamoja na wabunge kufurahia kusambazwa kwa vitabu vya kiada
vingi nchini, lakini anasikitika kwamba vitabu hivyo vina makosa mengi
katika uchapaji wake. Aliongeza kuwa, kutokana na vitabu hivyo kuwa na
makosa hayo, waliochangia kuchapisha vitabu hivyo, lazima watawajibika
kutokana na makosa hayo.
Alisema kwa watendaji wa TET ambao wanajiona hawana sifa ya kufanya
kazi hiyo hawana viwango katika kuandaa vitabu vyenye ubora, ni bora
wapishe na waiache taasisi hiyo. “Wale wote waliohusika na uchapishaji
vitabu ambavyo havina ubora watatakiwa kupewa adhabu kutokana na makosa
waliosababisha katika kuchapa vitabu hivyo,” alisema Prof Ndalichako.
Ndalichako alikiri kwamba vitabu hivyo vina makosa na serikali
imechukua hatua kuvirudisha na kuvirekebisha ili viwe katika ubora wa
kutumika katika kufundishia nchini. Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Suzan
Lyimo alisema, vitabu vipya vya kiada vya TET havina ubora na vina
upungufu mwingi.
“Vitabu hivyo vina upungufu mkubwa ambao usiporekebishwa unaweza
kusababisha madhara makubwa katika utoaji wa elimu na hivyo kushusha
ubora wa elimu yetu,” alisema. Lyimo alisema serikali inatakiwa
kuviondoa vitabu hivyo visitumike kwa ajili ya wanafunzi shuleni,
kutokana na ukweli kwamba vina makosa mengi.
Alisema, vitabu vya kiada vya shule ya msingi hasa darasa la kwanza
hadi la tatu na sekondari, vina makosa mengi ya usanifu, picha za vitabu
zimecheza na makosa ya lugha, kwa hiyo havina msaada katika kuelimisha
watoto.
Lyimo alisema vitabu vyote hivyo katika orodha havina viongozi wa
walimu, kukosekana kwa mwongozo huo, kunachangia walimu kutopatiwa
maelekezo na ufafanuzi au njia za kufundishia. Alisema kutokana na
vitabu vingi kuwa na makosa serikali inatakiwa kuviondoa visitumike,
japo serikali imetumika fedha nyingi kuvichapicha.
Vitabu hivyo vilianza kutumika mwaka jana na mwaka huu. Msemaji wa
Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Bashe alisema, serikali
inatakiwa kuboresha elimu ikiwa na pamoja kuhakikisha vitabu
vinavyoandaliwa kwa ajili ya wanafunzi vinakuwa katika ubora ambao
utasaidia kuboresha elimu nchini.
“Kamati inaishauri serikali kupitia wizara ya elimu ambayo ni mwenye
dhamana wa elimu nchini kuangalia upya mfumo wa elimu na kufanya mapitio
mazima na kuja na matokeo ambayo yataboreha elimu nchini kama taifa
linalotaka kuwa na uchumi wa viwanda,” alisema.
Alisema vitabu ambavyo vimechapishwa kwa lengo la kupunguza pengo la
vitabu vya kiada nchini, vimekuwa na makosa mengi yakiwamo ya
uchapishaji, usahihi wa lugha na havina kiongozi cha mwalimu.
Katika bajeti hiyo, Waziri wa Elimu aliomba bunge liidhinishe sh
trilioni 1.337 ambazo ni pungufu kwa asilimia 4.2 ya fedha ambazo
ziliombwa na kuidhinishwa katika bajeti ya mwaka 2016/17 ya sh trilioni
1.396.
Kamati iliomba kwamba serikali inatakiwa kuongeza bajeti ya wizara
hiyo ili angalau ifikie asilimia 10 ya bajeti kuu ya serikali ambayo ni
sh trilioni 31.699. Wakichangia bajeti hiyo, Mbunge wa Songwe, Philip
Mulugo (CCM) alisema kitendo cha wizara kuchapisha vitabu vyenye makosa,
linaitia doa serikali, inatakiwa kuangaliwa upya na watalaamu waliopo
katika Taasisi ya Elimu wanatakiwa kuangaliwa upya.
Mulugo aliyewahi kuwa naibu waziri katika wizara hiyo, alisema
anapenda elimu iwe bora, lakini kutokana na kuchapisha vitabu ambavyo
vimekosewa kunatia doa katika elimu ya Tanzania.
Mbunge wa Vunjo, James Mbatia alisema, Serikali lazima ichukue hatua
dhidi ya watu wanaotaka kuangusha elimu nchini, kwani bila kuwa na
vitabu bora ni vigumu kufikia malengo ya kuondoa ujinga nchini. Elimu
nchini Pamoja na matatizo hayo ya vitabu vilivyochapishwa Profesa
Ndalichako alisema Serikali imefanya vizuri katika kuboresha miundombinu
ya taasisi za elimu, shule za sekondari pamoja na ujenzi na ukarabati
miundombinu ya shule na vyuo mbalimbali nchini.
Pia imefanya vizuri katika ujenzi wa mabweni katika Chuo Kikuu Cha
Dar es Salaam (UDSM) ambayo watatumia wanafunzi 3,840 na kupunguza kama
si kuondoa kabisa tatizo la uhaba wa mabweni kwa wanafunzi wa chuo
hicho.
"Lakini pia imefanya vizuri katika ujenzi wa maktaba ya kisasa katika
chuo kikuu cha Dar es Salaam ambao unaendelea na utagharimu shilingi
bilioni 86.1 fedha hizo zinatolewa na Serikali ya China," alisema.
Aidha alisema Serikali imefanya vizuri pia katika kuongeza kiwango
cha mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ambapo bodi ya mikopo ilitoa
kwa wanafunzi 122,374 ambapo wanafunzi 28,785 ni wapya na wanafunzi
93,559 ni wanaendelea na masomo. Katika kipindi kifupi serikali imefanya
mambo mengi mazuri katika kuhakikisha elimu inaboreshwa nchini.
chanzo:habarileo.
Comments