
Ambayo
imetamka hivyo, kwa nia njema kabisa, na kwa lengo kubwa kwamba,
wananchi wake wa Zanzibar basi wawe sawa na wa mataifa mengine, juu ya
kupata na kutoa habari.
Kama
hivyo ndivyo, pia Rais wetu mpendwa wa Zanzibar wa awamu hii ya saba
dk: Ali Mohamed Shein, ni hivi karibuni tu amekemea tabia ya baadhi
watendaji wenye tabia ya kuwakimbia wandishi wa habari, kwa lengo la
kuficha habari.
Kwa
mwenye akili, hapo amefahamu kuwa kitendo cha kuficha habari sio
kizuri, maana pamoja na kukiuka Katiba, pia huwakosesha mambo kadhaa
wananchi ikiwa ni pamoja na kutofahamu nini kipo, nini kinakuja, nini
wanatakiwa wafanye au wajihadhari.
Wananchi
wetu, naamini wanategemea sana vyombo vyetu vya habari, kwa kupata
taarifa mbali mbali, tena hasa za maendeleo iwe za kiafya, elimu, siasa,
imani, utamaduni, michezo na hata juu ya mwenendo wa Serikali yao,
walioamua kuiweka madarakani.
Kama hivyo ndivyo, mbona
waandishi wa habari walioko Pemba, wamekuwa wakikoseshwa habari, na
kisha kuekewa vikwazo kadhaa na baadhi ya watendaji wakuu tena hasa wa
taasisi za Serikali na mashirika ya Umma.
Waandishi
wa habari walioko Pemba, wawatafsiri vipi watendaji hawa, au ofisi ni
milki yao, Katiba hawaifahamu, wanapuuza nukuu ya Rais wetu, hawajiamini
kuzungumza na waandishi wa habari, au ndio hao wanaodumaza upatikanaji
wa habari?
Zipo
taasisi za umma Kisiwani Pemba, watedaji wake tunaowaamini, wamekuwa
wakiwakwepa waandishi wa habari ,wakiwa na sababu zisizoingia akili mwa
biaadamu, na hasa kama wao ambao wamekabidhiwa madaraka kuziongoza
taasisi hizo kwa Pemba.
Kwa
mfano kikosi cha KMKM ,JKU, wizara ya Afya, wizara inayosimamia
wanawake na watoto unapotaka taarifa kwa mfano juu ya walikichokifanya
au malengo yao kwa mwkaa ujao, hapo ni shughuli kubwa na mtendaji wake
mkuu, huthubutu kusema kuwa hilo yeye halimuhusu.
Katika
kuficha kwao habari, hapo mwandishi ataambiwa kuwa kuna agizo kutoka
juu, habari zisitolewa na wala yeye sio msemaji, na kutakiwa mwandishi
wa habari alieko Pemba aende Unguja kwenye makao makuu ya taasisi hiyo.
Sasa
natujiulize, ni juu ipi kunakotoka agizo hilo, wakati kiongozi wetu
mkuu dk: Shein amesema kuficha habari sio sahihi na naamini na yeye
amenukuu sehemu ndogo tu ya katiba ya Zanzibar, kwa hilo hakukurupuka.
Inawezekana
wakuu wa vikosi hivi na mashirika mengine au wizara hizo zinazoficha
habari Pemba, sio lengo pengine ni hao wanaoitwa mabossi wakuu walioko
Unguja ndio waliowawekea kizingiti.
Ingawa
kwa hawa wanaoficha habari kwa mfano KMKM Pemba, hata ushirikiano
hawana, maana tulitarajia walau atoe namba ya simu ya huyo anaeitwa
bossi alieko Unguja, lakini hapo si hasa kukatiwa simu kabla ya
kuhitimisha mazungumzo.
Naamini
kwa hawa anaofanya ukiritimba wa kihabari Pemba, inawezekana kabisa
wanajua tu kuwa habari ni kwa ajili ya chakula kwa mwandishi, kwamba
akimkosesha atalala na njaa.
Laa…!!
hasha mwandishi wala hali habari, bali anachokitafuta ni kutekeleza
wajibu wake wa kuwahabarisha wananchi juu ya kazi na majukumu yaliofanya
na taasisi husika.
Hivi
sasa kwa mfano wizara ya Afya na ile inayosimamia wanawake na watoto,
kila unachohitaji humtaka mwandishi wa habari, aombe habari kwa njia ya
barua rasmi, ingawa wanasahau kuwa wao wanapowahitaji waandishi hao,
hunyanyua simu na kuwataka wafike pahala fulani ili kwenda kazini.
Au
sasa na waandishi wa habari nao wawafungie vioo, na mkiwataka walioko
Pemba, muende Ungua kwa wakuu wao kazi, mndhani hapo ndio itakuwa
tunawaweka wapi wananchi tunaowatumikia?.
Jamani
tunakwenda wapi, huu ndio utendaji wa kazi wa uwazi na ukweli au ni
sahihi mwandishi alieko Pemba kuvuuka maji hadi Unguja, ili apate habari
ambayo Pemba yupo mtendaji ambae tunaamini anaweza kutoa habari.
Tena
kwa sasa hata vile vituo vya mkono kwa mkono kwa mfano cha Chakechake
ambacho kilikuwa na urafiki mkubwa na waandishi wa habari, sasa
kimeshatiwa sumu kwamba ukihitaji baraua uende Wete kwa Afisa Mdhamini
kutaka ruhusa.
Taasisi
kama hizi zipo nyingi Kisiwani Pemba ambazo hudai kuwa zimepewa maagizo
ya maandishi kutoka kwa mabosi wao walioko Unguja, kwamba wasithubutu
kuzungumza na waandishi wa habari hata kwa lolote.
Jamani
tuwahurumie wananchi wetu wa Zanzibar hasa walioko Pemba, ili wapate
taarifa sahihi zilizomo kwenye taasisi zilizioko Pemba, au ndio
waendelee kuvipenda vyombo vya habari vya nje ya Zanzibar kwa kutoa
habari nzuri.
Watendaji wakuu waliopo Kisiwani Pemba ni vyema wakapewa ‘dozi’ washirikiane kikamilifu
na vyombo vya habari na waandishi wa habari walioko Kisiwani humo,
maana naamini migomo ya waandishi wa habari haina tija, lakini je na
sisi tukiamua kuwagomea maendeleo yatapatikana?
Mbona
bado kwa baadhi ya taasisi Kisiwani Pemba zinaendelea ukiritimba wa
kutoa habari kwa waandishi wa habari, tuseme hawa wako kwenye dunia
gani, au wakorofi ni wakuu wao waliopo makao makuu Unguja? siamani.
Inawezekana
wao hawa alioko Pemba wanataka kushirikiana na vyombo vya habari,
lakini kutokana na nidhamu ya waoga kwa mabosi wao, ndio maana sisi wa
mrengu wa habari, pengine tunawatupia lawama wao kwa kutokujua.
Lakini
mbona zipo taasisi hata Idara ndogo zinashirikiana vyema na vyombo vya
habari kwa mfano Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano, TRA, Shirika la
Utalii, Wizara ya Biashara, Katiba na Sheria, Ofisi ya Makamu wa Pili na
vitengo vyake na hata ZFA Pemba .
Hizi
naamini zote ni taasisi za Umma, na zina wakuu wake Unguja, sasa tuseme
kuzungumza na waandishi wa habari zinakikuka maadili, zinakikuka
maagizo ya mabosi wao, haziogopi waandishi wa habari, au ndo
zinazofahamu wajibu wao, jawabu ni kweli.
Hadi
lini taaisis hizi zitaendelea kuwa bubu kwa waandishi wa habari, na
kukosa taarifa sahihi za kuwapasha wananchi wetu, au ndio zinataka
waandishi wa habari waandike wapendavyo kisha iwe ni kunyosheena vidole,
hili sio jambo jema.
Mabosi
wa taasisi mbali mbali walioko Unguja wakati umefika sasa, kuwaamini
watendaji wenu wakuu walioko Pemba, na hasa kwa kile kinachohusu Pemba,
kwa nini wasikizungumze ili wananchi wakifahamu kupitia vyombo vya
habari.
Hili
la kukalia habari sasa limesharithishwa hata wa baadhi masheha wa
shehia, nao huuwaambia waandishi wa habari, kwamba wamekatazwa
kuzungumza chochote na vyombo vya hyabari hata kwa zile changamoto
zinazowakabili, wakidai kuwa hadi mwandishi apate ruhusa kutoka
Wilayani.
Lakini hili ka kuwafunga midomo
watendaji wasizungumze na waandishi wa habari, athari yake kamwe
haishii hapo bali kama ikiachiwa basi kuna siku hata wakuu wa Mikoa na
Wilaya wanaweza kuzuiwa wasizungumze na vyombo vya habari.
Sote
kwa pamoja, tunaweza pindi tukiamua kufanya shughuli na wajibu wetu kwa
kushirikiana na tena bila ya kusimamiwa, na mjenga nchi mwananchi
mwenyewe, ambao ni mimi na wewe.
chanzo:zanzibar24.
Comments