Uchafu wa Soko la Mabibo watoa ajira kwa Mwanadada Sarafina.

Wakiwa katika harakati za kujipatia maendeleo, Wanawake wengi barani Afrika wameendelea kujishughulisha katika kazi mbalimbali ili kujikomboa kiuchumi.

Mwanamke mmoja jijini Dar es salaam aliejitambulisha kwa jina la Sarafina anafanya kazi ya kuosha watu miguu nje ya soko la Mabibo mara tu wanapotoka kununua bidhaa mbalimbali katika soko hilo.

Mwanamke huyo anasema kuwa uchafu wa sokoni hapo ndio ulimpa wazo la kuanzisha biashara hiyo ambayo inamuendeleza kimaisha kwa kipindi hichi cha mvua.


Anasema kuwa mtu mmoja humnawisha kwa shilingi 100 na kwa siku huingiza kiasi cha shilingi elfu 30 na kufanikiwa kuajiri vijana wanne ambao wanamsaidia kufanya kazi hiyo sokoni hapo.
 chanzo:zanzibar24.

Comments