Pamoja na kudhibiti wizi huo, Waziri wa Elimu , Sayansi na
Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako alisema kwa sasa kuna udanganyifu
wa mitihani unaofanywa na walimu pindi mitihani inapofika kwenye vituo
vyao wanaichomoa na kuifanya kisha majibu kuwapa wanafunzi.
“Serikali bado tunajitahidi kufuatilia kwa karibu ili kudhibiti hali
hiyo, hivyo mfahamu wizi tumesha udhibiti wa mitihani isipokuwa huo
udanganyifu unaofanywa na walimu,”alisema.
Akizungumzia madeni ya walimu waliosimamia mitihani mwaka 2015 ambao
hajalipwa, Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi, Selemani Jafo alisema
deni hilo lilikuwa Sh bilioni 6.4, serikali imeshalipwa Sh bilioni
tatuna sasa deni limebaki Sh bilioni 3.4.
“Ni kweli walimu wanatudai na sasa deni lililobaki tushapeleka Hazina
wanalishughulikia na lipo hatua za mwisho hivyo karibuni Sh bilioni 3.4
zitalipwa,” alisema. Jafo alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge
wa Bukombe Doto Biteko (CCM) aliyeuliza lini serikali itawalipa walimu
waliosimamia mitihani mwaka 2015 ambao bado hawajalipwa hadi sasa.
Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Kahama Mjini, Jumanne Kishimba
(CCM) aliyeuliza kama serikali haioni umuhimu wa kumpima mwanafunzi kwa
kutathmini tangu shule ya msingi na kuoanisha mtihani wake wa mwisho
ilikupata uhalisia, Jafo alisema mfumo wa tathmini unaotumika kwa sasa
unajumuisha alama za upimaji wa mwanafunzi awapo shuleni na mtihani wake
wa mwisho.
“Mfano katika matokeo ya mtihani wa mwisho wa kitado cha nne, sita na
ualimu kwa cheti na Stashahada , alama za upimaji wa mwanafunzi awapo
shuleni zinachangia asilimia 30 na mtihani wa mwisho unachangia
asilimia70,”alisema.
Alisema serikali itaendelea kufanya utafiti kwenye mifumo ya utahini
inayotumika katika nchi mbalimbali duniani kwa lengo la kuboresha
mfumowa utahini kwa kadri itakavyoonekana inafaa na kwa kuzingatia
mazingira ya utoaji wa elimu bora nchini
chanzo:habarileo.
Comments