
Hayo yameelezwa na Afisa mkuu Idara ya maendeleo Uvuvi Pemba,
Sharif Mohammed Faki, katika mkutano wa
wafanyabiashara ya wavuvi wa Pweza, huko Weni Mkoa wa Kskazini Pemba.
Amesema kupitia mradi wa Swiofish unaoshughulika na masuala ya
uhifadhi wa samaki, kupitia kamati za wanavijiji kwa kufuta
utaratibu maalum wa viwango vya Pweza vilivyowekwa kulingana na sheria za Uvuvi
na sheria za maeneo ya hifadhi.
Sambamba na hayo, amesema kuwa, Serikali itaanzisha vituo vya
barafu ili kuhifadhi na kuanzisha viwanda vya kusarifu Pweza,kuwawezesha
wafanyabiashara waweze kuuza katika masoko ya ndani na nje, jambo ambalo
litasaidia kwa kiasi kikubwa kunyanyua biashara ya pweza nchini.
Akichangia katika mkutano huo, Mohammed Suleiman Ntale, ambae ni
mfanyabiashara ya Pweza katika Kampuni ya TANPESCA, ameiomba Serikali pia
kuangalia uwezekano wa kuwasaidia vifaa vitakavyowawezesha wavuvi kwenda
baharini na kupata Pweza wakubwa wenye viwango vinavyokubalika.
Nae Afisa usarifu wa mazao ya baharini, Nd. Juma Khamis Jafar,
amewataka wafanyabiashara hao kufuata taratibu za kisheria kwa kukata leseni na
hati miliki kwa wakati, ili kuepusha usumbufu katika harakati zao za kila siku.
Kwa sasa hifadhi ya Pweza ipo Mkoa wa Kusini katika Vijiji vya
Kisiwapanza na Kuukuu Kangani, na inategemewa hivi karibuni kuanzishwa katika
kijiji chaFundo katika Mkoa wa Kaskazini na utasimamiwa na Jumuiya ya Mwambao
na kuwa endelevuhadi kumalizika kwa maeneo ya Kisiwa cha Pemba.
Comments