Raia 45 wauawa katika mapigano Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Magenge ya waasi wanaobeba silaha katika Jamhuri ya Afrika ya Kati yameua makumi ya raia nchini humo katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.

Ripoti iliyotolewa leo Jumanne na shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch imesema kuwa, raia hao waliuawa katika makabiliano kati ya makundi hasimu ya waasi katika mkoa wa Ouaka, katikati ya nchi.


Lewis Mudge, Mtafiti wa masuala ya Afrika wa shirika hilo amesema watoto wanne wa familia moja akiwemo mtoto wa miezi saba ni miongoni mwa raia waliouawa mwezi Machi na kundi la wapiganaji wa Fulani Union for Peace in Central Africa.

Haya yanajiri siku chache baada ya Jeshi la Ulinzi la Uganda UPDF kuanza kuondoa askari wake huko Jamhuri ya Afrika ya Kati, ambao wamekuweko nchini humo tangu mwaka 2012.

Wanajeshi hao walikuwa miongoni mwa askari 3,000 wa Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, waliokuwa wakishirikiana na jeshi la Jamhuri ya Afrika ya Kati ambao wamekuwa wakiwasaka waasi wa genge la Kikristo la LRA akiwemo kiongozi wao Joseph Kony. 

Jamhuri ya Afrika ya Kati ilitumbukia katika mgogoro mwaka 2013 baada ya kuzuka mapigano ya kikaumu yaliyopelekea kuondolewa madarakani serikali ya Rais François BozizĂ©.
chanzo:parstoday.

Comments