
Sisi Hizb ut Tahrir Tanzania tunauliza, jee kikao cha siri hufanywa
ndani ya ukumbi wa hoteli ulioalikwa watu zaidi ya 450? Au kikao cha
siri kitaalikwa watu mbalimbali wakiwemo masheikh, maimamu, wasomi,
wanasiasa,
wanahabari, wanasheria, wanaharakati, wanamichezo nk?
Tunauliza zaidi, jee kikao cha siri hutangazwa ndani ya tovuti na
mitandao mbalimbali ya jamii waziwazi? Na kwanini taarifa za barua ya
kupiga marufuku ikatolewa siku moja kabla ya mkutano na kutuarifu sisi
masaa machache kabla ya kufanyika kongamano hilo?
Qadhia hii inafedhehi ziada juu ya dhulma, maonevu na mabavu ya mfumo
wa kidemokrasia kama inavyodhihirika kwa serikali zake duniani kote,
ambapo hudai kushikamana na kinachoitwa uhuru wa kuabudu na uhuru wa
maoni ilhali kiuhalisia matamshi hayo ni kauli mbiu za udanganyifu.
Kwa unyenyekevu mkubwa, tunawaomba radhi waalikwa wote kwa mashaka
yoyote yaliyowasibu kufuatia kuzuiwa kongamano hili adhimu lililokuwa na
lengo la kugusia masuala nyeti likiwemo la kufeli kwa mfumo wa kibepari
kilimwengu.
Aidha, kwa unyenyekevu tunawazinduwa kuwa qadhia hii ni
moja ya dhihirisho la waziwazi la kutoweza kumsimamia binadamu, kutofaa
na kukosa nishati kwa mfumo wa kibepari na nidhamu/system yake ya
kisiasa ya kidemokrasia, kwa kuwa vinamnyima mwanadamu kila kitu
ikiwemo hata fursa ya kufanya mjadala wa masuala nyeti.
Wakati umewadia kwa kila mwanafikra makini kutafiti mfumo mbadala
ambao bila ya shaka ni Uislamu na nidhamu yake ya kiutawala ya Khilafah
Na: Masoud Msellem,
Mwakilishi kwa Vyombo vya Habari
Hizb ut-Tahrir Tanzania.
chanzo: zanzibar24.
Comments