
Vifo hivyo vyote vimetokana na maporomoko ya maji, mawe, miti na
mchanga kutoka katika Milima ya Usambara Magharibi ambavyo vimeendelea
kuvamia kwa kasi baadhi ya nyumba zilizo mabondeni katika kata za
Mkumbara, Chekereni, Makuyuni, Kwagunda, Kerenge na Ngombezi.
Pia Imebainika kwamba hali ya usalama kwa baadhi ya wananchini mbaya
hasa wale wasiotaka kuhama kwenye nyumba zao zilizoko bondeni jirani na
kingo za Mto Pangani na kusababisha wanyama wakali akiwemo mamba
kuanza kuvamia nyumba hizo ili kutafuta malisho.
Akizungumza jana jioni katika mahojiano kwa njia ya simu, Mkuu wa
Wilaya ya Korogwe, Robert Gabriel alisema hali ya uslama kwa wakazi wa
maeneo hayo haijatengemaa hivyo jamii inapaswa kufanya kila
linalowezekana ili kuokoa maisha.
“Kuna tukio la kusikitisha sana la jana huko Kata ya Ngombezi ambako
ni jirani na mto Pangani kuna mama mmoja amenusurika kuliwa na Mamba
wakati alipokuwa akisafisha kifaa cha kudekia nyumba kwa kutumia maji
hayo ya mafuriko,”
Alisema mkuu wa wilaya na kuongeza: “Ilikuwa tu baada ya kumaliza
usafi akaamua kwenda kusuuza dekio bila kujua kwamba kumbe mamba alikuwa
mawindoni ametoka huko mtoni na kujichanganya kwenye hayo mafuriko
jirani na nyumba wakati mama akiendelea kusafisha ndipo mamba akavamia
hilo dekio na kuondoka nalo na mama akanusurika.”
chanzo:zanzibar24.
Comments