Mradi huo unaofadhiliwa na Benki ya Dunia mpaka utakapokamilika
utakuwa umegharimu Sh 1,039,000,000. Taarifa ya mradi huo ambao bado
kukamilika, zinasema kwamba mkandarasi Cosmos Engineering Co Ltd ambaye
ndiye anayejenga mradi huo ameshalipwa tayari Sh milioni 300 za awali.
Aidha, fedha nyingine Sh milioni 200, alilipwa lakini akanasa katika
tatizo la kodi ya serikali. Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge alisema wao
hawawezi kuweka jiwe la msingi la mradi kutokana na halmashauri kutotoa
vielelezo vya kutosha.
Kwa mujibu wa mkataba mradi ulipaswa kutekelezwa katika mwaka wa
fedha 2013/14 na kukamilika katika kipindi cha miezi sita.
Amour alisema
Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru imelea mkandarasi huo ambaye
anaonekana kuwa dhaifu katika utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa maji.
Amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Juma Homera kufanya uchunguzi
dhidi ya utendaji kazi wa mkandarasi Cosmos Engineering, kutokana na
kuonesha utendaji usioridhisha na kuchukua hatua za kisheria dhidi ya
watumishi wa halmashauri hiyo waliohusika.
Naye Mbunge wa Tunduru Kaskazini ambaye pia ni Naibu Waziri wa
Maliasili na Utalii, Ramo Makani amesema mradi wa maji wa Matemanga
umekuwa na changamoto nyingi tangu uanze kutokana na fedha kuchelewa.
Pia alisema mkandarasi ameonekana kutokuwa na uwezo wa kifedha wa
kuendesha mambo yake akisuburi malipo ya serikali. Awali, Halmashauri ya
Wilaya ya Tunduru iliwahi kuvunja mkataba na mkandarasi Cosmos kwa kile
kilichoelezwa ni kushindwa kutekeleza mradi huo mwaka 2016.
Hata hivyo, katika mazingira yanayotia shaka halmashauri hiyo Aprili
2017 ilimwongezea mkataba wa miezi miwili mkandarasi huyo na kutakiwa
akamilishe mradi ifikapo Juni 2017 kitu ambacho kiongozi huyo wa mbio za
Mwenge alisema hapendezwi nacho.
CHANZO:habarileo.
Comments