Madereva wa gari za mchanga wategewa misumari- Donge chechele.

Watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana wametega misumari nadani ya madimbwi ya maji pamoja na kufunga njiaianayoelekea shimo la mchanga Donge chechele.

Madereva wa gari za mchanga ambao ndi waathirika wakubwa wa tukio hilo wamesema, hawakuridhishwa na hatua iliyofanywa na watu hao  kutokana na kuwasababishia hasara ya magari yao kutoboka mipira kutokana na misumari hiyo.


Hivyo madereva hao wameiomba serikali ichungeze ili kuwatia mikononi watuo hao wanaowatia wasiwasi wa usalama wa maisha yao.

Nae msimamizi mkuu wa mashimo ya Mchanga Dole chechele Abubakar Mussa Ali amekilaani sana kitendo hicho na kusema kuwa wanajipanga vizuri na wanahakikisha kuwapata watu hao ambao ni maadui wa watu na mali zao.

chanzo: zanzibar24.

Comments