Mabadiliko ya hali ya hewa Zanzibar ndio chanzo cha miundombinu kuharibika.

zanzibarSerikali ya Mapinduzi Zanzibar imetakiwa  kushirikiana na Asasi za kiraia  katika  kuelekeza nguvu zao  ili kukabilaina na mabadiliko ya tabia ya nchi  kwani kunauwezekano mkubwa kwa Zanzibar kupoteza eneo lake kubwa la ardhi.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika mafunzo ya siku moja ya athari za mabadiliko ya tabianchi  Mratibu wa Mradi  wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianch Zanzibar
ZACCA Soud Mohammed Juma amesema kutokana na  utafiti uliofanyika Zanzibar kunauwezekano mkubwa wa kupoteza ardhi yake  jambo linalisababishwa na mabadiliko ya  hali ya hewa  na kuharibu miundombinu  pamoja na kupoteza eneo lake la kilimo.
Hata hivyo amesema  hali ya toto zanzibar imeongezeka kutokana na hali hiyo serikali iyoneumuhumi  kutilia mkazo suala hili kwa  kutoa elimu zaidi kwa wananchi kuwacha kuchimba mchanga,kukata miti,kuvamia maeneo hatarishi kwani itapelekea athari kubwa kwa wananchi hasa wanyonge.
Aidha waandishi wa habari kwa nafasi zao wametakiwa kuelimisha umma juu ya mabadiliko ya tabianch na athari zake kwani kuna mifano hai imeanza kujitokeza  ikiwemo upepo mkali ya kimbunga,Mafuriko,maji ya bahari kuvamia makaazi ya wananchi pamoja na  maeneo ya kilimo.
Kwaupande wao baadhi ya waandishi wa habari walioshiriki mafunzo hayo Amina  Mchezo na Ali Abdallah wamesema licha ya jitihada zinazochukuliwa za kuwaelimishwa jamii kupitia vipindi mbalimbali katika vyombo vya habari tatizo kubwa ni ukosefu wa ajira hupelekea jamii kuvamia maeneo hatarishi kwa kufanya shughuli zao za maisha ili kujikimu ikiwemo ukataji wa kuni,uchomaji wa mikaa,uchimbaji wa mchanga  lakini serikali ikiwasaidia vijana kuwa wezesha tatizo hilo litapungua.
chsanzo:Zanzibar24

Comments