Kipindupindu chaingia Zanzibar, 23 waripotiwa kuugua.

Wizara ya afya Zanzibar imepiga marufuku uuzwaji wa Vyakula usiozingatia utaratibu wa kiafaya katika jamii kutokana na kujitokeza kwa vimelea vya ugonjwa wa kipindupindu katika baadhi ya Maeneo ya Zanzibar.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mjini Zanzibar Kaimu waziri wa afya Riziki Pembe Juma amesema maeneo yalijitokeza kuwepo na vimelea hivyo ni pamoja na maeneo ya wilaya ya magharib A na B na Wilaya ya Mjini ikiwemo Daraja bovu,Kinuni,Chumbuni,Fuoni na Mtoni kidatu.


Kaimu waziri amesema jumla ya wagonjwa ishirini na tatu (23) wameripotiwa kuugua ugonjwa huo kutoka maeneo hayo tangu kuanza kwa ugonjwa huo mwishoni mwa mwezi march mwaka huu.

Aidha amesema kutokana na kuibuka kwa maradhi ya matumbo na vimelea vya ugonjwa wa kipindupindu wizara ya afya imewataka wafanya biashara walioruhusiwa kufanya biashara zao kufuata taratibu za kiafya ili kuepuka kusambaza vimelea hivyo kwa wateja wao.
Kaimu Waziri wa Afya Zanizbra, Bi. Riziki Pembe Juma akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Dk. Jamala (mwenye miwani) na Mkurugenzi kinga na elimu ya afya Dk. Fadhil Muhammed
Nae mkurugenzi kinga na elimu ya afya Dk. Fadhil Muhammed amesema mbali na kupiga marufuku vyakula vinavyouzwa kinyume na taratibu za kiafya lakini pia si vyema kwa wananchi kuendelea na mikusanyiko wakati wa futari hususan katika kipindi hichi cha mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Jumla ya wagonjwa Efu 4 mia 3 na 30 waliugua ugonjwa wa kipindu pindu kati yao 68 walipoteza maisha katika kipindi cha mwaka 2016 ,ambapo kwa mwaka 2017 jumla ya wagonjwa 23 wameanza kuugua ugonjwa huo.

chanzo:Zanzibar24.

Comments