Kampeni ya Mimi na Wewe kujenga madarasa 52 Mkoa wa Mjini Magharibi.

Mkuu wa  mkoa wa mjini Magharibi Ayoub Mohammed  Mahmoud amesema kampeni ya mimi na wewe imekusudia kuhakikisha ujenzi wa  madarasa 52  katika mkoa wake yanakamilika ili kupunguza  msongamano  wa wanafunzi  katika madarasa.

Akizungumza na Waandishi wa habari katika ukumbi wa Rahaleo amesema kuelekea kwenye uzinduzi wa kampeni ya mimi na wewe  itakayo anza kesho kwa matembezi ya amani na kufuatiliwa  na uchangiaji  wa damu salama, kutakua na zoezi la ujenzi wa madarasa 52  yaliyopo katika ngazi mbalimbali  zikiwemo za msingi, kozi nne  na paa yatakamilika ili kuwawezesha watoto  wa mkoa huo kusoma katika mazingira mazuri.


Akizungumzia swala la uchangiaji damu salama  amesema  zoezi hilo limekusudia  kupunguza upungufu wa tatizo la damu kwa wagonjwa  wanaohitaji huduma hiyo  hasa katika kipindi cha mwezi mtukufu wa ramadhani .

Hata hivyo  amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi hapo kesho katika harakati mbalimbali zitakazo fanyika ili kuipa sapoti serikali katika hatua zake za kuwaletea wananchi maendeleo ya haraka na kusema kuwa  kampeni ya mimi na wewe inalenga kuwarejesha wananchi katika uzalendo wa kizanzibar  na kuwachana na ubaguzi  ambao unaleta mifarakano katika jamii.

Aidha amesema baada ya kukamilika kwa kazi zote zilizokusudiwa katika kampeni hiyo pia kutakuwa na uchangiaji  wa vitu mbalimba kwa viongozi ambapo vitu hivyo viwasaidia makundi mbalimbali wakiwemo wasio jiweza,wazee mayatima,kaya maskini pamoja na watu wenye ulemavu.

Kampeni hiyo inatarajiwa kuzinduliwa na Makamo wa Rais Samia Suluhu Hassan hapo kesho katika viwanja vya mnara wa kumbukumbu  Mapinduzi Squea kisonge.
chanzo:Zanzibar24

Comments