Bwawa hilo halitahusu kilimo kikubwa cha umwagiliaji kwani serikali
itaangalia uwezekano mwingine wa kuweka miundombinu wezeshi ya kilimo
cha umwagiliaji kulingana na maeneo husika.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Isaack Kamwelwe alisemaSerikali
imetenga Sh bilioni 1.5 kwa mwaka wa fedha 2016/2017 na imepanga kutenga
Sh bilioni mbili kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya fidia
kulingana na tathmini iliyofanywa.
“Serikali inaandaa malipo ya fidia kwa mujibu wa sheria yaardhi ya
mwaka 1999 ambayo inaelekeza pia kuwa endapo malipo ya fidia yatachelewa
kulipwa kwa zaidi ya miezi sita tangu kupitishwa, mlipaji
atapaswakufanya mapitio na kulipa nyongeza na muda uliozidi,”alisema.
Kamwelwe alikuwa akijibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Morogoro
Kusini Mashariki, Prosper Mbena(CCM) aliyetaka kufahamu kama serikaliipo
tayari kuboresha malipo ya fidia kwa wanavijiji wote walioathirika kwa
nyumba na mashamba yao kuchukuliwa kupisha ujenzi wa bwawa la maji
Kidunda nakama serikali ipo tayari kwenye bajeti hii kumalizia malipo ya
takriban Sh bilioni 3.7 kuwafidia wananchi hao kulingana na tathmini
iliyofanyika.
chanzo:habarileo.
Comments