
Msimamo huo ameutoa wakati akikagua shamba la CCM lenye zaidi ya
hekta 200 huko katika Kijiji cha Kilombero Wilaya Kaskazini “B” Unguja,
alisema CCM haiwezi kufikia dhamira yake ya kuimarika kiuchumi endapo
kama kuna baadhi ya watu wanaotumia rasilimali hizo kwa maslahi binafsi.
Alisema lengo la CCM kupitia mabadiliko ya muundo wa taasisi hiyo
yaliyofanyika hivi karibu ni kuhakikisha rasilimali zinatumika vizuri na
kwa maslahi ya wengi kwa lengo la kufikia dhamira chama hicho
kujitegemea kiuchumi.
Dkt. Mabodi alisema CCM itasimamia Utekelezaji wa Ilani yake ya
Uchaguzi ya mwaka 2015/2020 kama ilivyowahidi wananchi kwa kuhakikisha
inaondosha mianya yote ya ubadhirifu wa mali za chama hicho.
![]() |
Ni msafara wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Abdalla Juma Saadala na baadhi ya wananchi wakiongozwa na Viongozi wa CCM Wilaya ya CCM Kaskazini “B”, wakikagua shamba hilo. |
Hata hivyo alifafanua kwamba atashirikiana kikamilifu na chombo
kilichopewa dhamana ya kusimamia rasilimali zote za CCM ambacho ni
Baraza la Wadhamini kwa lengo la kukagua mali hizo na kutatua kasoro
zilizopo ili kuongeza ufanisi ndani ya taasisi hiyo.
“ CCM tuna mashamba ya kilimo cha kisasa hivyo natoa wito kwa vijana
wetu badala ya kudai ajira kutoka serikali na katika makampuni pia
watumie fursa za kilimo kujiajiri wenyewe kwani nchi yetu ina soko kubwa
la mazao ya kilimo hasa katika Mahoteli ya kitalii.”, alitoa Wito kwa
Vijana Dkt. Mabodi.
Naibu Katibu Mkuu huyo akizungumzia malalamiko ya baadhi ya wamiliki
wa maeneo yaliyopakana na shamba hilo wanaodai kumiliki baadhi ya miti
ya miembe na vipande vya ardhi katika eneo hilo, aliwaruhusu waendelee
kuvuna maembe hayo huku CCM ikijadili njia bora ya kumaliza tatizo hilo.
![]() |
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Abdalla Juma Saadala akishauriana masuala mbali mbali na baadhi ya wananchi wakiwa ndani ya shamba hilo. |
Pia Dkt. Mabodi alisifu juhudi za Wasisi wa ASP walionunua shamba
hilo kwa njia ya kuchangishana fedha ili litumike kwa ajili ya makaazi
ya wananchi waliokuwa hawana sehemu za kuishi baada ya ardhi zao
kudhurumiwa na utawala wa kimabavu uliotawala Zanzibar kabla ya
Mapinduzi ya Mwaka 1964.
Aliwasihi vijana wa sasa kufuata nyayo za waasisi hao kwa kuhakikisha
wanalinda na kuanzisha vitega uchumi vipya na rasilimali za kudumu za
CCM ili viweze kubaki kama kumbukumbu ya kujivunia na kuvinufaisha
vizazi vijavyo.
Aidha Dkt. Mabodi aliwataka wafugaji wa kijiji hicho kuacha tabia za
kulisha mifugo yao katika mashamba ya wakulima hasa wa Zao la mpunga,
kwani kufanya hivyo ni kuchochea migogoro isiyokuwa ya lazima.
Pia aliuagiza uongozi wa CCM Wilaya hiyo kuhakikisha katika shamba
hilo hapajengwi nyumba na miradi ya kudumu ya watu binafsi sambamba na
kulinda wananchi wanaoishi katika eneo hilo mpaka pale chama kitakapokaa
na kufanya maamuzi ya mwisho yatakayojali utu na haki za wananchi hao.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa kijiji hicho, walisema
matarajio yao baada ya ziara hiyo ni kutatuliwa kwa haraka changamoto
zinazowakabili.
![]() |
Moja ya maeneo ya wananchi yaliyolimwa mpunga yaliyopo katika shamba hilo. |
Naye mkaazi wa kijiji hicho , Juma Vua aliwasihi viongozi wa Chama na
Serikali kuiga utamaduni wa Naibu Katibu Mkuu huyo Dkt. Mabodi kwa
kuwatembelea wananchi katika maeneo yao ili kujionea kero na changamoto
zinazowakabili kwa lengo la kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.
Shamba hilo ambalo ni miongoni mwa urithi wa waasisi wa Afro Shiraz
Party(ASP) walionunua rasilimali hiyo toka mwaka 1953 kutoka mikononi
mwa mmoja wa viongozi wa kisultani kwa ajili ya wananchi waliokuwa
wakiishi bila ya makaazi ya kudumu waishi katika eneo hilo baada ya
kunyang’anywa ardhi yao na utawala wa wakati huo.
chanzo:zanzibar24.
Comments