Duru za kuaminika za Jamhuri ya Afrika
ya Kati zimetangaza habari hiyo na kuongeza kuwa, hatua ya kuwarejesha
nyumbani wanajeshi 500 wa Uganda waliotumwa mashariki mwa nchi hiyo
kutawasababishia matatizo ya kiusalama na kiuchumi wakazi wa eneo hilo.
Operesheni ya kuwarejesha nyumbani wanajeshi wa Uganda waliotumwa
kupambana na magaidi wa LRA huko Jamhuri ya Afrika ya Kati inamalizika
mwishoni mwa mwezi huu wa Mei.
Duru hizo za Jamhuri ya Afrika ya Kati
zimesema kuwa, viongozi wa mji wa Obo wa mashariki mwa nchi hiyo
hawajawa na uwezo wa kulinda usalama wa maeneo hayo na kuna hatari mji
huo ukakumbwa na mashambulizi ya waasi wa Kikristo wa LRA, baada ya
kuondoka wanajeshi wa Uganda.
Ukiachana na masuala hayo ya kiusalama,
kuweko wanajeshi wa Uganda huko Jamhuri ya Afrika ya Kati kumekuza pia
uchumi wa mji wa Obo hasa kwa vile wafanyabiashara wa mji huo walikuwa
wakitoa bidhaa zao Sudan Kusini kutokana na kuweko usalama katika eneo
hilo.
Hata hivyo kuondoka wanajeshi wa UPDF mjini humo kutasababisha
matatizo makubwa ya kiusalama na pia ya kiuchumi.
chanzo: parstoday.
Comments