Akielezea kinachomsumbua baba yake mtoto wa Mzee Sozigwa, Mchungaji Moses Sozigwa alisema tatizo la kwanza lililokuwa likimsumbua baba yao ni kupoteza kumbukumbu.
Mchungaji Sozigwa alisema baadaye ilikuja kubainika ana tatizo la moyo, madaktari walisema moyo wake umekuwa mkubwa.
“Tunasubiri vipimo vingine tufahamu zaidi kinachomsumbua, nafikiri vitatoka leo (jana)au kesho (leo) kwa sababu pia amekuwa akilalamika kuumwa tumbo,” alisema Mchungaji Moses Sozigwa.
Comments