
Akikabidhi msaada huo mkurugenzi mipango wa jumuiya hiyo Mussa Ali
Buruki amesema jumuiya hiyo imekuwa ikijishughulisha na masuala mbali
mbali ya kijamii ikiwemo kujenga Miskiti pamoja na uchimbaji wa visima.
Akipokea msaada huo Afisini kwake Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba
Mwanajuma Majid Abdalla ameitaka jumuiya hiyo kuendelea kuwa na
mshikamano kwani bado misaada zaidi inahitajika.
Kwa upande wao waathirika wa maafa hayo ambao walikabidhiwa msaada
huo wameomba kusaidiwa ujenzi wa nyumba zao ambazo zimeharibika vibaya
na hata nyengine kuanguka kabisa.
Comments