Afariki Dunia kwa kuzama ndani ya bwawa la maji – Kandwi.

Kijana mmoja amefariki Dunia hapo jana majira ya saa 4 asubuhi  baada ya kuzama katika bwawa la maji alilokua akiogelea katika kijiji cha Kandwi Wilaya ya Kaskazin A Mkoa wa kaskazini Unguja.

Kaimu kamanda wa Polisi ambae pia ni mkuu wa wa upelelezi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Suleiman Hassan Suleima Amemtaja Marehemu huyo kuwa ni Foum Eme Khamis (23) Mkaazi wa Kandwi Mkoa wa kaskazini Unguja.


Kaimu kamanda huyo ametoa wito kwa jamii kuwa makini na kuchukua tahadhari wakati wanapokoga maji ya aina kama hiyo.

Mwili wa marehemu huyo umefanyiwa uchunguzi katika hospitali ya Kivunge na kukabidhiwa jamaa zake kwa mazishi.

 chanzo:zanzibar24.

Comments