
Hitma hiyo, ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa,
Rais mstaafu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Ali Hassan Mwinyi Rais
Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Awamu ya Sita, Mhe. Amani
Abeid Karume na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd.
Viongozi wengine walihudhuria katika hitma hiyo ni Mufti Mkuu wa
Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabhi, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis
Haji, viongozi wa serikali zote mbili na viongozi wastaafu, viongozi wa
vyama vya siasa, Masheikh kutoka Zanzibar na Tanzania Bara, Wabunge na
Wawakilishi, wananchi kutoka sehemu mbali mbali pamoja na Mabalozi
wadogo waliopo hapa Zanzibar.
Hitma hiyo ya kumuombea dua Marehemu Mzee Abeid Amani Karume pia ni
miongoni mwa maadhimisho ya Siku ya Mashujaa ilitanguliwa na Qur-an
tukufu, iliyosomwa na Ustadh Sharif Muhidin na kuongozwa na Sheikh
Mohammed Kassim Said kutoka Kamisheni ya Mufti na Mali ya Amana.
Mara baada ya hitma hiyo, Sheikh Juma Faki Chum alitoa mawaidha na
kumuelezea marehemu mzee Abeid Amani Karume kuwa ni kiongozi
aliyepigania maendeleo ya wananchi wa Zanzibar na kumuombea
MwenyeziMungu ampe makaazi mema Peponi.
Baada ya kisomo hicho cha hitma ambacho hufanyika kila mwaka
inapofika tarehe 7, Aprili, viongozi hao na wananchi waliohudhuria
katika hitma hiyo walimuombea dua, marehemu mzee Abeid Karume katika
kaburi lake lililopo pembezoni mwa afisi hiyo ya CCM Kisiwandui dua
iliyoongozwa na viongozi wa dini tofauti akiwemo Mufti Mkuu wa Zanzibar
Sheikh Omar Kabhi wka upande wa dini ya Kiislamu, Askofu Augostino Shayo
kutoka Kanisa Katoliki Jimbo la Zanzibar na Kashap Pandra aliyesoma kwa
niaba ya Wahindu.
Viongozi na wanafamilia waliweka mashada ya maua katika kaburi la
marehemu mzee Abeid Amani Karume akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan aliyeweka shada la
maua kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia, ni
Amiri Jeshi Mkuu Dk. John Pombe Magufuli, Kombo Mzee Kombo aliyeweka
shada la maua akiwakilisha wazee.
Wengine walioweka shada la maua ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya
Tanzania Jenerali Venance Salvatory Mabeyo, Balozi Ali Karume aliyewek
kwa niaba ya familia ya Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume na Balozi
mdogo wa Msumbiji anayefanya kazi zake hapa Zanzibar Jorge Augusto
Menezes aliyewawakilisha Mabalozi wenzake wa hapa nchini.
Aidha, Mama Mwanamwema Shein aliungana na akina mama wengine katika
hitma hiyo iliyofanyika katika Afisi hiyo ya CCM Kisiwandui, akiwemo
mjane wa marehemu mzee Abeid Karume, Mama Fatma Karume, Mama Shadya
Karume na viongozi wengine wanawake wa kitaifa wakiwemo Mawaziri,
Wabunge, Wawakilishini na wananchi kutoka sehemu mbali mbali ya Zanzibar
na Tanzania Bara.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya hafla hiyo, Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa aliwasisitiza
wananchi kuimara umoja na mshikamano sambamba na kuimarisha Mungano
uliopo ambao umeasisiwa na viomhozi Wakuu wa Taifa hili akiwemo Marehemu
Mzee Abeid Amani Karume na Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
April 7, 1972 ndiyo siku aliyouawa Rais wa Kwanza wa Zanzibar
marehemu Mzee Abeid Amani Karume na wapinga maendeleo nchini ambapo hivi
leo imetimia miaka 45 tokea utokee msiba huo.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
chanzo@:zanzibar24.
Comments