Wizara ya afya yapanga kuwafikisha mahakamani wanaopinga juhudi za kutokomeza Malaria.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatarajia kutumia chanjo ya Malaria ili kutokomeza ugonjwa huo ifikapo mwaka 2023 .

Afisa wa Afya kutoka kitengo cha malaria Mwinyi Issa Khamis amesema chanjo hiyo inayofanyiwa majaribio na Shirika la afya Duniani ,katika nchi tano za Africa ikiwemo Kenya ,Burundi na Malawi iwapo italeta mafanikio itaweza kutumika Zanzibar katika kutokomeza ugonjwa hatari wa Malaria.


Akizungumza katika Maadhimisho ya siku ya malaria nchini amesema wakati Zanzibar inasubiri matokeo ya Majaribio hayo kitengo cha kumaliza maria kinafanya tathmini juu ya njia zitakazotumika kumaliza ugonjwa wa malaria nchini.

Nae Naibu waziri wa Afya Zanzibar Harusi Saidi Suleiman amesema Zanzibar tayari imekuwa na mulekeo mazuri wakumaliza malaria na tayari imesha anzishwa sheria maalumu itayowabana watu wote ambao wanapuuza taratibu za kiafya juu ya kujinga na kutokomeza ugonjwa huo.

Aidha amesema Wizara ya afya imekusudia kuwafikisha mahakamani wananchi wanaopinga juhudi za serikali katika kutokomeza Malaria wakiwemo wananchi wanaokataa kupigiwa dawa bila sababu za Msingi.

Katika kipindi cha mwaka jana watu watano wamefariki dunia kutokana na kuugua Ugonjwa hatari wa malaria kati ya Watu waliougua ugonjwa huo.
chanzo:Zanzibar24.

Comments