WFP yalaani mauaji ya wafanyakazi wa ufikishaji misaada ya kibinadamu Sudan Kusini.

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakuka Duniani (WFP) limelaani muaji ya wafanyakazi wake watatu wanaohudumu nchini Sudan Kusini.

Taarifa iliyotolewa na WFP imeashiria kuwa katika shambulio la hivi karibuni la watu wenye silaha katika mji wa Wau magharibi mwa Sudan Kusini raia wasiopungua 16 pia wameuawa na kusisitiza kwamba shirika hilo lina wasiwasi kutokana na machafuko na umwagaji damu unaoendelea kushuhudiwa nchini humo.

Shirika la Mpango wa Chakula Duniani vilevile limeeleza masikitiko yake kwa kuuliwa watu ambao wanafanya jitihada kwa ajili ya kuawasaidia mamilioni ya raia wa Sudan Kusini na kutaka maisha ya watu hao yalindwe.
Taarifa ya shirika hilo la Umoja wa Mataifa imeongeza kuwa watu wapatao elfu nane wakaazi wa mji wa Wau wamelazimika kuzihama nyumba na makazi yao na kuwa wakimbizi kutokana na kuendelea mapigano na machafuko katika mji huo.
Tangu mwaka 2013 Sudan Kusini inashuhudia vita na mapigano ya umwagaji damu baina ya waungaji mkono wa Rais Salva Kiir na wanamgambo watiifu kwa aliyekuwa makamu wake na ambaye pia ni kiongozi waasi, Riek Machar.
chanzo:parstoday.

Comments