
Sabra Zubeir Makame na Halima Juma Ali
wamesema watu wenye ulemavu wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya
udhalilishaji na kesi inapofikishwa mahakamani hukosekana ushahidi
kutokana na hushindwa kujielezea kulingana na ulemavu wao.
Akijibu malalamniko hayo Mrajis wa Mahakama kuu Zanzibar George Kazi
amesema kesi za watu wenye ulemavu zimekuwa zikisikilizwa kwa umakini
zinapofikishwa mahakaman ili kila mmoja haki yake iweze kupatikana.
Aidha George ametoa wito kwa jamii iwapo wanakesi ambazo hazijapatiwa
ufumbuzi hasa za watu wenye ulemavu kwenda mahakamani kutoa taarifa ili
kupatiwa haki zao na watuhumiwa wa kesi kuweza kuchukuliwa hatua za
kisheria.
chanzo: Zanzibar24.
Comments