
Washtakiwa waliopewa hukumu hiyo ni Ame Hassan Ame (27) mkaazi wa Pita na Zako, Heri nyambuto nyangata (25) makaazi wa kijichi, Fidha Mohd Said (21) mkaazi wa kijichi na John Ilyas Moris (35) mkaazi wa Bububu.
Imedaiwa mahakamani hapo na muendesha mashtaka wa polisi Sajent Hassan Mussa Mshamba mbele ya hakimu Nassir Faki Mfaume kuwa siku ya tarehe 3 mwezi wa 4 majira ya saa moja asubuhi huko kujjichi bila ya halali wamepatikana wakiwa wamezidi ndani ya Gari yenye namba za usajili Z956 AWW yenye ruti namba 120 ikitokea upande wa Bububu Polisi na kuelekea Mndo jambo ambalo ni kosa kisheria.
Baada ya kusomewa kosa hilo washtakiwa walikiri bila ya kuwa na shaka lolote ndipo walipopewa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwao na wengine wenye tabia kama hiyo.
chanzo:zanzibar24.
Comments