Taarifa zilizolifikia gazeti ili kwa nyakati tofauti zinaonesha
wanafunzi hao wa elimu ya msingi na sekondari walitoweka kati ya Oktoba
mwaka jana na Februari mwaka huu.
Hata hivyo, Mkuu wa wilaya hiyo, Estomiah Chang’ah amehusisha tatizo
hilo na wanafunzi wanaopata mimba na kisha wazazi hutoa visingizio vya
wanafunzi hao kupotea.
Wanafunzi watatu ambao ni Consolata Chibuga wa darasa la saba Shule
ya Msingi Kakerege na Judis Kayumba wa darasa la pili Shule ya Msingi
Nakoza na Nisawa Abubakar wa kidato cha pili Shule ya Sekondari
Nakatungulu wametoweka tangu Oktoba 17, mwaka jana.
Wakati huo, Muhailwa Dotto ambaye ni mwanafunzi wa darasa la nne wa
Shule ya Msingi Mulezi alitoweka Januari 29, mwaka huu na Gloria
Majaliwa wa darasa la pili Shule ya Msingi Kakerege alitoweka Februari
25, mwaka huu.
Juma Mazigo anasema mtoto wa shemeji yake, Gloria (13), ametoweka tangu Februari 25, mwaka huu na hadi sasa hajulikani alipo.
Alisema siku hiyo, Gloria alitoroka na kulala kwa shangazi yake,
Lucia Nyakalonge baada ya mkewe ambaye ni mama yake mdogo, kutishia
kumpiga kwa sababu ya kukaidi maelekezo yake na siku iliyofuta aliaga
kurudi nyumbani, lakini akaenda kusikojulikana.
Walimu wakuu wa shule hizo wamethibitisha wanafunzi hao ni watoro wa
muda mrefu huku Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kakerege, Diamond Msita
anasema juhudi za kuwatafuta wanafunzi hao ili warudi na kuendelea na
masomo zinaendelea.
chanzo:Habarileo.
Comments