Wakaazi wa Chaani waiyomba serikali kuwatengezea barabara ili waweze kuondokana na matatizo yayowakabili.

chaaniWakaazi wa chaani wameiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwatengenezea barabara inayoanza Chaani kikobweni mpaka Gamba  ili waweze kuondokana na matatizo yayowakabili  wakati wa safari hususani kwa mama wajawazito.

Wakizungumza na Zanzibar24 Wakaazi hao na madereva wa njia hiyo wamesema kwa kipindi kirefu wamekabiliwa na tatizo hilo bila kupatia ufumbuzi jambao linalosababisha kuzorota kwa maendeleo  kijijini hapo.


Hata hivyo wamesema mara kwa mara wamekuwa wakiwatumia viongozi wao wa jimbo kuwaombea katika serikali juu ya kujengwa kwa barabara hiyo lakini mpaka sasa hawajaona matumaini ya kujengwa kwa njia hiyo.

Aidha wamesema pindipo serikali itakuwa msatari wa mbele katika kuijenga njia hiyo itwasaidi vijana kuondokana na tatizo la ukosefu wa ajira linalosababishwa na ubovu wa Barabara kutokana na  kushindwa kusafirisha biadhaa mbalimbali wanazo zalisha ikiwemo bidhaa za kilimo kupeleka katika masoko.

wakikabiliwa na tatizo la ubovu wa barabara bila ya kupatiwa ufumbuzi.
chanzo: Zanzibar24.

Comments