Wafugaji wa samaki Pemba watakiwa kuyatumia mabwaya yao kwa ajili ya mkendeleo.



Related imageMSAIDIZI afisa mkuu  idara ya maendeleo ya uvuvi Pemba Bi Mayasa Hamad Ali amewataka wafugaji wa samaki kuacha kuyageuza mabakuli ya kuombea misaada  mabwawa ya samaki bali wayatumie kwa ajili ya maendeleo ya uchumi  katika familia zao.

Akizungumza na wafuygaji wa samaki huko katika ukumbi wa mikutano weni , amesema ni vyema kwa wafugaji wa samaki kuyatimia mabwawa hayo kwa ajili kuongeza uzalishaji ambao utawasaidia kimaisha.

Amesema wafugaji wa samaki wamekuwa na tabia ya kuyatymia mabwawa kwa kuombea misaada kwa wafadhili jambo ambalo halileti pia nzuri .

Akiwasilisha taarifa ya hali halisi ya ufugaji wa samaki , afisa ufugaji wa mazao ya baharini Pemba Mohammed Salimu Othman amesema ufugaji wa samaki umeshuka kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo wizi pamoja na ukosefu wa vifaranga .

Mapema akifungua mkutano huo , afisa mkuu wa Idara ya maendeleo ya uvuvi pemba , Ndg Sharif Mohammed Faki amewataka wafugaji kuweka mazimngira ya mabwawa yao katika hali ya usafi ili kukidhi vigezo vinavyohitajika wakati huu ambapo serikali inajiandaa kutoa vifaranga vya samaki kwa wafugaji .

Comments