Wafanya biashara Zanzibar watakiwa kufuata sharia za afya kuepuka miripuko ya maradhi.

HABARIMkurugenzi  kinga na Elimu ya Afya Zanzibar  Dokta Fadhil Mohammed ametoa  onyo  kwa wafanyabiashara  watakao  kiuka taratibu na sheria za afya zilizowekwa katika kipindi hichi cha mvua za masika kuzifungia  biashara zao ili kuepusha  Miripuko ya maradhi ya kipindupindu.
Akizungumza na Mwandishi wa Zanzibar24 huko Ofisini kwake amewataka wafanyabiasha kuhakikisha biashara zao zipo katika maeneo salama ilikulinda afya za walaji  na kufata masharti ya afya.

Hata hivyo amesema maradhi ya miripuko Zanzibar bado yapo na kuna maeneo hatarishi ikiwemo                  Chumbuni, Daraja bovu, Bweleo, Fumba, Matemwe,  Kiwengwa,  Upenja hadi Kilombero na upande wapemba ni Kojani,Wete,Chake vitongoji na Michezani wananchi wachukue tahadhari sana kwa kuzidisha usafi katika maeneo yao na kuchemsha maji ya kunywa pamoja na kunawa mikono kabla ya kula.
Amesema sababu kubwa ya maradhi ya kipindupindu kujitokeza mara kwa mara  nipale wananchi wanapokosa maji katika maeneo yao na kupelekea kutumia maji ya vidimbwi pamoja na uchafuzi wa mazingira.
Chanzo:Zanzibar24

Comments