Alitaka hivyo baada ya Wakili wa Serikali, Patrick Mwita kudai kuwa kesi hiyo imekuja kutajwa.
Alisema wanaahirisha kesi hiyo kwa muda mfupi ili kutoa uamuzi sahihi
kutokana na mabishano ya kisheria kati ya upande wa mashitaka na
mawakili wa utetezi kuhusu kufunguliwa upya kwa kesi hiyo.
Aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 11, mwaka huu kwa ajili ya kutoa
uamuzi. Mawakili wa utetezi walidai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kinyume
cha sheria, hivyo ifutwe.
Awali, washitakiwa Mrita na Muyela waliachiwa huru na mahakama hiyo
mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa kisha wakakamatwa tena na
kusomewa upya mashitaka ya mauaji.
Katika kesi hiyo, washitakiwa hao wanatuhumiwa kumuua kwa makusudi
Aneth Msuya ambaye ni dada wa bilionea Erasto Msuya. Mauaji hayo
yanadaiwa kutendeka eneo la Kibada, Kigamboni jijini Dar es Salaam, Mei
25, mwaka jana.
Wakili wa washitakiwa, Peter Kibatala aliiomba mahakama kufuta kesi
hiyo akidai kuwa imefunguliwa kinyume cha sheria, kwani ilishafutwa.
Alidai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kinyume cha sheria kwa sababu
ilishatolewa uamuzi Februari 23, mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi,
Godfrey Mwambapa aliyewaachia huru washitakiwa wote.
Aidha, alidai kuwa mahakama hiyo haikuwa na mamlaka ya kulipokea
jalada hilo na kuwasomea washitakiwa mashitaka yao kwa kuwa
limeshatolewa uamuzi.
Hata hivyo, Wakili wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi alipinga hoja hizo
na kudai kuwa washitakiwa wamesomewa kosa hilo kwa mujibu wa sheria.
Alidai kuwa uamuzi uliotolewa ulikuwa ni kuwafutia mashitaka ambapo
Jamhuri ina uwezo wa kuwakamata tena washitakiwa na kuwasomea kosa hilo
la mauaji.
Pia haoni sehemu yoyote ambayo inaonesha kosa walilosomewa washitakiwa lipo kimakosa mahakamani hapo.
chanzo:Habarileo.
Comments