Ukosefu wa kanuni maalum katika benki kwapelekea kudumaa kwa uchumi.

benkiUkosefu wa kanuni maalum ambazo zitaziwezesha Benki za kiislam nchini kufanya shughuli zake kama sheria inavyotaka inazikosesha fursa ambazo zingeweza kupatikana kwa benki hizo katika kusaidia ukuwaji wa uchumi.

Akizungumza na Mwanahabari wetu mtaalam wa masuala ya uchumi hapa Zanzibar Dk.Mohammed Hafidh Khalfan ambae hivi karibuni ametunukiwa tuzo ya mshauri bora wa masuala shariah na taasisi ya Alhuda Center of Islamic banking and Economics iliopo Dubai.


Amesema kukosekana kwa kanuni hizo hivi sasa benki hizo zimekuwa zikifanya kazi katika mazingira magumu kutokana kutegemea kanuni za benki za kawaida.

Hata hivyo Dk.Mohammed amesema kinachokosekana hivi sasa kwa mashehe hao ni kuweza kuunganisha taaluma zao kisharia walizozisoma na taratibu za kifedha ili kuwa na mchango mzuri katika sekta hiyo.

Aidha ameitaka jamii kuzitumia ipasavyo benk za kiislam bila kuzingatia itikadi zao za dini kwani benki hizo zipo kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wote.
chanzo: Zanzibar24.

Comments