
Hayo yameelezwa na Kaimu Afisa wanyamapori wa wilaya ya Tunduru Bw.Limbega Hassan aliyeongoza kikosi cha askari wanyamapori waliokuwa wakiangalia usalama wa tembo na wananchi ambapo wananchi wamemng’oa meno mawili tembo mmoja na kuondoka nayo huku meno mawili ya tembo mwingine yakisalimishwa kituo cha polisi cha Tunduru.
Kaimu Afisa wanyamapori huyo wa wilaya ya Tunduru anasema kuwa wamewakamata watu watano wanaodaiwa kuhusika na kuwaua tembo wawili na kutoweka na meno huku wekiwatafuta wengine wawili wawachukulie hatua na pia mikakati ikiwekwa kuwadhibiti tembo katika vijiji vitano vinavyosumbuliwa na tembo.
Hata hivyo pamoja na makundi makubwa ya tembo kuingia kwenye vijiji na kuleta taharuki mkuu wa wilaya Tunduru Bw. Juma Homera amesema kuwa hali ya usalama iko shwari askari wanyamapori wamefanikiwa kuwadhibiti tembo hao na hakuna mwananchi aliyedhurika.
chanzo:Muungwanablog.
Comments