Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira),
January Makamba, aliyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati akifungua
Mkutano Mkuu wa Nne wa mpango huo ulioandaliwa na Korea na Benki ya
Dunia.
January alisema pamoja na Korea kuwa na maendeleo makubwa ya viwanda,
lakini imekabiliana na uharibifu wa mazingira kupitia mpango huo na
kupunguza hewa ukaa.
Alisema katika kuelekea uchumi wa viwanda ndani ya miaka 10 ijayo,
nchi inaweza kuwa mstari wa mbele katika kuleta ‘Green Growth’ kupitia
mikakati bora na sera ya rasilimali.
chanzo:Habarileo.
Comments