
Uongozi huo umekutana na Watendaji wa Tume ya Udhubiti wa Dawa za
Kulevya pamoja na wale wanaosimamia udhibiti wa uhalifu Chini ya
Mwenyekiti wake Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Nd. Ahmad Kassim Haji Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.
Mshauri wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Shirika la Umoja wa Mataifa
linaloshughulikia mapambano dhidi ya uhalifu na Dawa za kulevya { UNODC }
Bibi Sylvie Bertrand alisema mpango huo wa Mafunzo utashirikisha Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar.
Bibi Sylvie alisema katika kuupanguvu zaidi mpango huo ili ufanikiwe
vyema Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto pia
itakuwa mshirika katika mpango huo utaoratibiwa na Tume ya Kudhibiti
Dawa za Kulevya Zanzibar.
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
6/4/2017.
chanzo: zanzibar24.
Comments