Simba imetangaza kuwa tayari imelipa kodi iliyokuwa inadaiwa na
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) baada ya kuingiza nyasi bandia nchini
ambazo zilikuwa zimeletwa kwa ajili ya kuwekwa katika uwanja wa Simba
uliopo Bunju Dar es Salam.
Katika taarifa ambayo imetolewa na Simba SC kupitia akaunti yake ya
Instagram imesema tayari imelipa kodi na nyasi hizo kwa sasa zitapelekwa
Bunju kwa ajili ya kuwekwa katika uwanja ambao itakuwa inautumia
kufanya mazoezi.
“Taarifa Rasmi kuhusiana na Nyasi Bandia, Mpaka sasa Tumeshalipia
Kodi yote ya Nyasi Bandia, Kinachoendelea sasa ivi ni Wakala wetu
kumalizia taratibu za Kutoa Container zenye nyasi hizo bandarini kwenda
kuwekwa rasmi katika uwanja wetu wa Bunju.”
chanzo:zanzibar24.
Comments