Serikali yataka vyombo vya habari kufuata na kutii sheria za nchi.

Vyombo vya habari nchini vinamchango mkubwa kuelimisha jamii na kusaidia kuleta maendeleo  na kuimarisha amani na utulivu nchini .

Akizungumza katika kikao kilichowakutanisha wamiliki wa vyombo vya habari, watendaji wakuu wa vyombo hivyo na wajumbe wa kamati ya maendeleo ya  wanawake habari na utali ya baraza la wawakilishi Zanzibar Mwenyekiti wa kamati hiyo Ally Suleiman Shihata amesema ili kuimarisha maendeleo zaidi ni vyema kwa vyombo hivyo kufuata sheria za nchi zilizopo.


Kwa upande wao Baadhi ya wamiliki wa vyombo hivyo  wamesema utozwaji wa kodi za kulipia minara ya kurushia matangazo,  kutopewa uhuru wa  nafasi za kurusha matangazo ya moja kwa moja  kutoka katika matukio ya kitaifa na viongozi kutotoa mashirikiano mazuri kati yao ni miongoni mwa matatizo yanayokwamisha maendeleo ya habari.

 Nae waziri wa habari utalii utamaduni na michezo Rashid Ally Juma,amesema mkutano huo umeongeza mwamko wa ushirikiano baina ya vyombo vya habari na serikali katika kuihudumia jamii na kuongeza kasi ya upatikanaji wa taarifa .
chanzo:Zanzibar24.

Comments