Serikali kuajiri jumla ya walimu wapya 3,081 mwaka huu.

Kulingana na uhaba wa walimu Mashuleni Serikali imeajiri walimu wapya 3,081 ambao wametakiwa kuripoti kuanzia Aprili 18, 2017.

Imeelezwa kuwa baada ya kutolewa nafasi hizo bado kuna nafasi nyengine za walimu 1,048 zilizotolewa kibali cha ajira kutoka kwa walimu.


Waziri wa TAMISEMI, George Simbachawene amesema kuna upungufu wa walimu 26,026 wa masomo ya sayansi na hisabati na kuna ziada ya walimu 7,463 wa masomo ya sanaa nafasi ambazo zitatakiwa kujazwa.
chanzo: zanzibar24.

Comments