Hata hivyo, bandari hiyo ambayo inaelezwa kuwa itasaidia kupunguza
msongamano wa malori katika Jiji la Dar es Salaam, inatarajia kuanza
kutoa huduma Julai mwaka huu, baada ya kukamilika hatua ya pili ambayo
ni ujenzi wa miundombinu mingine ndani ya bandari hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Deusdedit
Kakoko aliliambia gazeti hili kuwa kazi ambayo Suma JKT walikabidhiwa
wameshaikamilisha na sasa hatua inayofuata ni ujenzi wa miundombinu
mingine ndani ya bandari hiyo kavu.
“Nina imani kuwa shughuli zote zitakamilika hivi karibuni na bandari
hiyo itaanza kutoa huduma zake mwezi Julai,” alisema Kakoko. Alisema
ujenzi wa majengo ndani ya bandari hiyo kavu utafanywa na kampuni ambazo
zitaiendesha ICD hiyo.
Alisema kwa sasa TPA inaangalia uwezekano wa kuingia ubia na
wawekezaji wa sekta binafsi katika kujenga majengo ndani ya eneo hilo na
kuiendesha.
Alisema pia kuwa ili kuleta ufanisi, TPA inafikiria kuwahusisha sekta
binafsi ili wagawiwe maeneo ndani ya eneo hilo ili waiendeshe kwa
pamoja.
Alisema hata hivyo suala hilo litatekelezwa iwapo atapata baraka za mamlaka za juu za serikali.
Mkurugenzi huyo alisema ujenzi mwingine utakaofanyika katika eneo
hilo ni wa tuta la reli na ujenzi wa reli yenyewe ambao utatoka ilipo
Reli ya Kati na kuunganisha na bandari hiyo kavu.
Alisema ujenzi wa tuta wataufanya Suma JKT wakati ujenzi wa reli utafanywa na kampuni inayojenga miundombinu ya Reli.
Alisema tayari TRL imeshatoa mchoro wa ujenzi wa reli hiyo na wanasubiri gharama za ujenzi wa reli hiyo pamoja na tuta.
“Kwa sasa ndio kwanza tunataka kwenda kufanya majadiliano, hatujajua
gharama halisi za ujenzi wa reli hiyo,” alieleza mkurugenzi huyo.
Mwanasheria wa JKT, Kanali John Mbungo alisema kazi waliyokuwa wamekabidhiwa wameshaikamilisha na zimebaki shughuli ndogo ndogo wanazoendelea kuzikamilisha.
Alitaja kazi hizo kuwa ni kusafisha eneo hilo la ekari 500 kwa kufyeka msitu, kusakafikia ardhi na kushindilia kokoto.
Alisema kazi hiyo ilikuwa ni kubwa, lakini kwa kuwa wana utaalamu
mkubwa walifanikisha ujenzi huo wa awali ndani ya muda waliopewa na
serikali.
Alisema Suma JKT ingefurahi kama ingepewa zabuni nyingine ya kujenga majengo ndani ya ICD hiyo.
“Sisi kwa kweli kazi yetu tumekamilisha, ila kuna kazi ya kujenga
majengo ndani ya eneo hilo, tungefurahi kama wangetupatia kazi hiyo,
lakini kwa sasa hatujui nani atapewa,” alieleza Kanali Mbungo.
Akizungumza wakati wa kutia saini makubaliano ya ujenzi wa ICD hiyo,
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa
alisema ujenzi wake unalenga kupunguza msongamano wa malori jijini Dar
es Salaam na
ungekamilika ndani ya wiki tisa.
ungekamilika ndani ya wiki tisa.
Profesa Mbarawa alisema ujenzi wa ICD hiyo utagharimu Sh bilioni 7.3
na utakapokamilika, makontena yote yatapelekwa kwenye bandari hiyo ya
Ruvu kwa reli na malorii yanayotoka mikoani na nchi jirani yatakuwa
yanachukulia mzigo wake katika huko badala ya kuja Dar es Salaam.
chanzo:Habarileo.
Comments