Rais atoa zawadi za Pasaka kwa watoto wenye mahitaji maalum.

 Rais John Magufuli ametoa zawadi zenye thamani  ya Shilingi 11.7milioni   katika vituo tisa tisa vya watoto wenye mahitaji maalum mkoa wa Dar es Salaam.

Vituo vingine vilivyofaidika na zawadi hizo ni viwili vya Zanzibar na 21 vya kwenye mikoa ya Tanzania bara.
Taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari Maelezo inaeleza kuwa Kamishna wa Ustawi wa Jamii, Rabikira Mushi alikabishi zawadi hizo kwa niaba ya Rais.
Mushi alisema utoaji wa zawadi hizi umekuwa ni utaratibu wa kawaida kwa  Rais Magufuli ambapo alitoa zawadi za vyakula kama vile mchele, mbuzi na mafuta ya kupikia ili kuwawezesha makundi yenye mahitaji maalum kufurahi na kusherehekea sikukuu kama ilivyo kwa watu wengine.
Baadhi ya vituo vilivyofaidika na zawaidi hizo kwa mkoa wa Dar es Salaam na Zanzibar  ni,Makao ya Taifa ya Watoto Yatima Kurasini,Makao ya Watoto Mburahati,Makao ya Watoto Msimbazi.Makao ya Watoto Kijiji cha Furaha,Makao ya Watoto SOS Children’s Village Tanzania.
chanzo:Mwananchi.

Comments