WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amesema wizara yake
inafuatilia kwa karibu kubaini watekaji na watu wanaokamata na
kuchukuliwa watu wengine nchini.
Kauli hiyo aliitoa mjini Dodoma wakati wa mahojiano na vyombo vya
habari nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya wabunge kuitaka serikali itoe
tamko kutokana vitendo ya utekaji na kuchukuliwa watu kuendelea
kujitokeza nchini.
“Tayari wizara yangu inashughulikia suala hilo la kutekwa msanii Roma
Mkatoliki na kuchunguza ili kuona ni nani anahusika katika utekaji huo,
kwani anaweza kuwa asiwe askari na mtu mwingine akatumia mavazi ya
askari kufanya utekaji huo,” alieleza Mwigulu.
Mwigulu alisema kama serikali kupitia wizara yake inatakiwa kufanya
mambo kwa uhakika pamoja na kuchunguza ndipo itoe taarifa kuhusu jambo
lolote.
Alisema tayari wizara yake imechukua hatua za kuchunguza jambo hilo la msaniii Roma.
Ndani ya Bunge wakati wakichangia Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu,
wabunge waliuliza kwanini serikali inanyamaza kimya kutoa tamko wakati
wimbi la kutekwa watu na kukamatwa na kupotea bila kueleweka wapo wapi
linaendelea kutokea nchini.
chanzo:Habarileo.
Comments