Philemon alidai hayo wakati
wakiongozwa na Wakili wake, Nehemiah Nkoko mbele ya Hakimu Mkazi, Huruma
Shaidi, kujitetea katika kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi
inayomkabili pamoja na, raia wa China ‘Malkia wa Pembe za Ndovu’, Yang
Feng Glan (66) na Salvius Matembo.
Philemon alidai kuwa Aprili 20,2014 alikamatwa maeneo ya Njia Panda
ya Segerea wakati akienda kununua vinywaji kwa ajili ya biashara yake ya
Motel.
Alidai kuwa baada ya kukamatwa alipelekwa Kituo cha Polisi
Stakishari na kuchukuliwa na askari polisi, Sajenti Beatus na kupelekwa
Kituo cha Polisi Oysterbay ambapo askari huyo aliwataka vijana wawili
waandae mazingira ya kumning’iniza mshitakiwa huyo kama popo.
Aliieleza mahakama kuwa alimhoji Beatus ni kwanini ameanza vitisho
ambapo askari huyo alianza kumuandikia maelezo yake ikiwemo biashara
yake ya ufugaji, kilimo, moteli na madini ya ng’ombe.
‘’Afande Beatus
nilimkabidhi simu mbili na Sh milioni 2.6 kisha aliagiza vijana wale
wawili waje ambapo walikuwa na bomba, wakanifunga pingu miguuni na
mikononi kunifunga pamoja miguu na mikono kwa kutumia bomba na kunifunga
bandeji mdomoni ambapo nilining’inizwa kwenye meza kama popo miguu juu
kichwa chini na kunipiga kwa kutumia rungu kwa saa 3,’’ alidai Philemon.
Mshitakiwa huyo alidai kuwa baadaye alifunguliwa pingu na kuulizwa
kama yupo tayari kuendelea kutoa maelezo yake ambapo alimwambia kuwa ana
hali mbaya kwa kuwa anajisikia kizunguzungu. Pia alidai kuwa Beatusi
alimchukua na kumpeleka polisi Kijitonyama ambapo aliwekwa rumande.
Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 5, mwaka huu kwa ajili ya
kutoa uamuzi wa kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi kama mshitakiwa huyo
aliteswa ama la.
Kesi hiyo ndogo ndani ya kesi ya msingi imeanza kusikilizwa baada ya
Wakili wa upande wa utetezi, Jeremiah Mtobesya kupinga maelezo ya onyo
ya Manase yasipokelewe kama kielelezo cha kesi hiyo mahakamani kwa
sababu aliyatoa polisi na yalichukuliwa nje ya muda na alipigwa na
kunyanyaswa.
Washtakiwa hao wanadaiwa kuwa kati ya Januari Mosi, 2000 na
Mei 22, 2014 kwa makusudi raia wa China, Yang Feng Glan aliongoza na
kufadhili vitendo vya kijinai kwa kukusanya na kusafirisha vipande hivyo
706 vya meno ya tembo bila ya kuwa na kibali chochote kile kutoka kwa
Mkurugenzi wa Wanyamapori.
Kwa upande wa washtakiwa Salvius na Manase
wanadaiwa kuongoza makosa ya uhujumu uchumi kwa kusaidia biashara ya
nyara za serikali kwa kukusanya, kusafirisha na kuuza meno ya tembo kwa
nia ya kujipatia faida.
chanzo:Habarileo.
Comments