
Akizungumza katika mkutano uliowakutanisha Viongozi wakuu wa
Mashirika ya umoja wa mataifa UN nchini na Viongozi wa Hospitali ya
mnazi mmoja kuangalia maendeleo na Matatizo yanayoikumba hospital hiyo
amesema mbali na kuimarisha kwa jengo la kina mama na watoto lakini
wanashindwa kufikia malengo kutokana na kukabiliwa na tatizo la uhaba wa
wauguzi.
Hata hivyo amesema katika kufikia lengo walilolikusudia jumla ya
wauguzi mia mbili hamsini wanahitajika ili kupunguza tatizo hilo pamoja
na kuweza kurahisisha huduma za wauguzi kwa kina mama wanao hitaji
huduma hizo wakati wa kujifungua.
Kwa upande wake Afisa kutoka Shirika la umoja wa kimataifa Batul Abdi
amesema katika kupunguza matatizo yanayoikabili hospiatal hiyo ni vyema
kwa Serikali ya Zanzibar kuandaa utaratibu wa kuajiri wafanyakazi
watakaoziba nafasi za wauguzi ili kupunguza vifo vya kina mama na watoto
vinavyojitokeza mara kwa mara.
Wakati huo huo Daktari Mkuu wa Hospital ya Mnazi Mmmoja Zanzibar
Dk.Nuofal Kassim Muhammed amesema mbali na kuwepo kwa tatizo hilo ujio
wa wageni hao umeonesha kuridhika kwa jitihada mbalimbali
zinazochukuliwa na serikali na uwongozi wa hospital hiyo kwa kufikia
hatua ya kuweza kujitegemea katika utendaji wao wa kazi.

chanzo:Zanzibar24.
Comments