Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar imesema itahakikisha inasimamia
azma yake ya kudhibiti uvuvi haramu Bahari kuu ili kuweza kufaidika na
uchumi unaotokana na mazao ya baharini.

Akizungumza mara baada ya kuwasili kwa meli ya doria hapa Zanzibar
inayotoka Madagaska ambayo inaelekea katika ukanda wa bahari kuu
kwaajili ya doria Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya kusimamia Uvuvi
haramu wa Bahari mkuu Hosea Gonza Mbilinyi amesema kutokana na hasara
inayopatikana wamejipanga kikamilifu kuhakikisha wanawadhibiti wavuvi
harama katika ukanda wa bahari mkuu ikiwa lengo ni kupiga vita uvuvi
haramu na uwepo wa meli hiyo itasaidia kupunguza uvuvi harama.

Hata hivyo amesema Tanzania inashirikia na nchi mbalimbali ikiwemo Madagaska, Komoro, Muzambique, Kenya,
Morishaz, Msumbiji na Shelisheli kwa na lengo la kudhibiti uvuvi harama
bahari kuu ambapo wamedhaminiwa chini ya ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya
IOC.

Doria hiyo ya kudhibiti uvuvi haramu ulianza mwezi huu wanne tarehe
11 hadi tarehe 8 mwezi wa 5 ambapo kila nchi inachangia asilimia 20 hadi
30 za gharama za uwendeshaji wa zoezi hilo.
chanzo:Zanzibar24
Comments