Mashahidi
30 wa upande wa mashtaka wanatarajiwa kutoa ushahidi Mahakama Kuu katika
kesi ya mauaji ya kukusudia ya aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko
ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi.
Wakili wa Serikali, Patrick Mwita alisema hayo jana alipowasomea washtakiwa Msigwa Matonya, Mianda Mlewa, Paulo Mdonondo, Longishu Losingo, Juma Mayunga na John Mayunda wanaokabiliwa na kesi hiyo maelezo ya mashahidi walioshuhudia tukio hilo na vielelezo ambavyo vitatumika wakati wa usikilizwaji wa shauri hilo.
Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakili Mwita alisema watakuwa na vielelezo 13 ikiwamo ramani ya tukio na ripoti ya daktari kuhusu kifo cha Dk Mvungi.
Washtakiwa hao wanadaiwa Novemba 3, 2013 katika eneo la Msakuzi Kiswegere lililopo wilayani Kinondoni walimuua kwa kukusudia Dk Mvungi.
chanzo:Mpekuziblog.
Comments