Alitoa pongezi hizo wakati akihutubia baraza hilo kwenye Makao Makuu
ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani hivi karibuni.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa Dar es Salaam
na wizara hiyo, Balozi Mahiga aliyewakilisha nchi 15 za SADC,
aliipongeza UN kwa ujumla chini ya uongozi wa Katibu Mkuu, Antonio
Guterres kwa kuongeza muda kwa Monusco na jitihada nyingine nyingi za
kutafuta suluhu ya kudumu kwa changamoto mbalimbali zinazoikabili DRC
kwa muda mrefu ikiwemo ukosefu wa amani na usalama.
Alisema kupitishwa kwa azimio hilo kunatoa matumaini mapya kwa
wananchi wa DRC na dunia kwa ujumla kwamba UN ina nia ya dhati
kuhakikisha amani ya kudumu inapatikana nchini humo.
Aidha, alitumia nafasi hiyo kuiomba UN kutambua mchango mkubwa
unaotolewa na Kikosi Maalumu cha Force Brigade Intervention- FIB
kilichoundwa na SADC ambacho kinashirikiana na Monusco katika ulinzi wa
amani DRC.
FIB ina mchango wa vikosi vya ulinzi wa amani kutoka nchi tatu za SADC ambazo ni Tanzania, Afrika Kusini na Malawi.
chanzo:Habarileo.
Comments