
Kumekua na lalama dhidi ya kiongozi huyo baada ya wanawe watatu
kugunduliwa wanamiliki akaunti za siri kufuatia ufichuzi wa stakabadhi
za Panama.
Bwana Sharif na familia yake wamekanusha kuvunja sheria yeyote na kusema kesi ya sasa imechochewa kisiasa.
Serikali
imesema ina imani Mahakama ya Juu itamuondolea lawama Waziri Mkuu. Kesi
dhidi ya Waziri Mkuu imevutia hisia tofauti nchini humo pamoja na
kutawala taarifa za magazeti.
Mahakama ya Juu ilikubali kumchunguza bwana Sharif baada ya kiongozi wa upinzani Imran Khan kutishia kuongoza maandamano.
Inadaiwa pesa kutoka akaunti hiyo ya siri zilitumiwa kununua nyumba mjini London Uingereza.
Sharrif amesema nyumba hiyo ilinunuliwa kwa njiya halali.
Hata
hivyo wakosoaji wake wamesema akaunti hizo za siri zinatumika na Waziri
Mkuu na familia yake kuwepa kodi pamoja na kuvukisha fedha
zilizopatikana na njiya haramu.
Mahakama ya Juu inaweza kuamrisha uchunguzi zaidi dhidi ya Waziri Mkuu na hata kumuachisha kazi.
Stakabadhi za Panama zilifichuliwa kutoka kwa kampuni ya wanasheria ya Panama Mosaack Fonseca.
Kampuni
hiyo imekua ikiwasaidia wanasiasa na wafanyibiashara kuwa na akaunti za
siri katika mataifa ya nje hasa visiwa vya mbali. Akaunti hizi
hazionyeshi wamiliki wake halisi .
chanzo:Bbc.
Comments